Jumamosi, 14 Aprili 2018

Maraisi wa vyama vya wanasheria wapatikana

ad300
Advertisement

Wanasheria kutoka Chama cha Wanasheria wa Tanganyika(TLS) kwa umoja wao leo wamemchagua wakili Fatma Karume kuwa Rais mpya atakayekiongoza chama hicho.
Fatma Karume anachukua nafasi ya Mwanasheria mwenzake Tundu Lisu ambaye amemaliza muda wake.


Hii ni baada ya kuwagaragaza wagombea wenzie  watatu ambao ni, Simba Ngwilimi, Musa Mwapongo na Godfrey Wasonga.


Wakati kwa upande wa  Zanzibar wanasheria wa Nzanzibar wamemchagua
Wakili Omar Said Shaaban kuwa Rais Mpya wa chama cha Wanasheria Zanzibar(ZLS).


Awali Rais wa TLS anayemaliza muda wake TunduLissu aliwatakia  kira raheri Mawakili katika uchaguzi wa leo, kuchagua viongozi wenye uwezo wa kuendesha taasisi hiyo kwa uhuru bila kuingiliwa.


Huku akiwataka  mawakili hao kuwakataa wagombea watakaoathiri uhuru wa TLS kwa kushirikiana na maadui wa Utawala wa Sheria.


Katika uongozi wake Lissu amefanikiwa kutekeleza mambo makubwa matatu;
1) Kuanzisha mchakato wa Ujenzi wa Ofisi ya Makao Makuu ya TLS.


2) Kupunguza ada za Mawakili.


3) Kufumua mfumo wa usimamizi wa fedha wa taasisi hiyo ambayo ilikuwa ikituhumiwa kwa matumizi mabaya.


Ushindi huu unamfanya Fatma kuingia kwenye historia ya kuwa mwanamke wa pili kushika nafasi hiyo toka kuanzishwa kwa chama hicho cha mawakili  zaidi ya miaka 60 iliyopita. Rais wa kwanza wa TLS mwanamke ni Judge Joaquine De Melo




Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 maoni: