Jumatano, 18 Aprili 2018

Dondoo za soka barani ulaya

ad300
Advertisement

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho anataka kumsaini kiungo wa kati  Mbrazil Fred kutoka Shakhtar Donetsk ili kujaza nafasi  inayoachwa na mchezaji Paul Pogba.

Real Madrid inahitaji kumpata mchezaji wa kimataifa Mfaransa paul pogba lakini rais wa  timu hiyo Florentino Perez hawezi kusaini mchezaji mwenye Umri kuanzia  miaka 25.Labda apunguze mahitaji yake ya mshahara na aoneshe kiwango  kizuri kwenye michuano ya Kombe la Dunia. (Express)

Manchester City inampango wa kumpata mshambuliaji wa Ufaransa anaekipiga katika klabu ya  Paris St-Germain Kylian Mbappe, mwenye umri wa miaka 19, na kiungo wa Bayern Munich, Thiago Alcantara Mwenye umri we miaka 27 na wote wanatarajiwa kutua  Etihad msimu huu. ( Skyports)

Mchezaji wa Uingereza anayecheza katika klabu ya  Norwich, James Maddison, mwenye umri wa miaka 21, anahitajika na  vilabu kadhaa vya Ligi Kuu, ikiwa ni pamoja na Tottenham, Arsenal, Everton na Manchester City. (Telegraph)

Borussia Dortmund anataka  kupata saini ya mchezaji  Michy Batshuayi kwa mkopo kutoka klabu ya  Chelsea,  wakati wa majira ya joto. Chelsea inataka zaidi ya £ 50m kwa mchezaji huyo wa  ubelgiji mwenye umri wa miaka 24.

Chelsea inataka kumsaini mchezaji wa Nice Jean Michael Seri kwa ada ya £ 35m, lakini mchezaji wa kimataifa wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 26 anatarajiwa kusubiri na kuona ni nani atakuwa mmiliki wa the Blues msimu ujao. (Mirror)

Luke Shaw bado hajafanya uamuzi kuhusu maisha yake ya baadaye huko Manchester United. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 ataamua hatima yake  mwishoni mwa msimu, baada ya kuwa na uhusiano mgumu na meneja  wa manchester united Jose Mourinho. (ESPN)

Barcelona inahitaji kuwa na hadi £ 60m ili kumpata mshambuliaji wa Manchester United Anthony Martial mwenye umri wa miaka 22, na Ryan Sessegnon mwenye umri wa miaka 17 kutoka  Fulham. imeeleza klabu hiyo kupitia email yake

Liverpool na Tottenham walikuwa miongoni mwa timu  pande zote za Ligi Kuu ya Uingereza zilizotuma waangalizi wake  kumtazama winger wa Benfica kutoka nchini  Serbia na Andrija Zivkovic katika mchezo  wa  Premier ligi  dhidi ya  Porto. (The sun)

Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 maoni: