Jumatatu, 26 Februari 2018

Watakaofanya Maandamano kukiona cha mtema kuni

ad300
Advertisement

Polisi kanda maalumu ya Dar es salaam  imetoa onyo Kali kwa wale wanaohamasisha na watakaoshiriki maandamano.

Akizungumza na waandishi wa habari kamanda kanda maalum jijini Dar es salaam Lazaro Mambosasa amesema

Nawaomba watanzania wapenda amani wajiepushe na mpango wa watu wachache wa kuingiza nchi kwenye vurugu, ninachotaka kusema yeyote atakaeshindwa kuyapokea haya ninayosema asijutie kitakachomkuta"

Aidha Mambosasa amewaomba watanzania kudumisha hali ya amani  na kujiepusha na Maandamano yanayopangwa kufanyika

"Kuna watu wanaendelea kuwahamasisha wananchi wafanye maandamano halafu wanafanya hivyo wao wakiwa wamekaa mahali salama, sasa nataka niwaambie watanzania mtu anaejua thamani ya amani ajiepushe na kwa kanda ya Dar es salaam atakaefanya maandamano asijutie yatakayotokea"

Mbali na taarifa hiyo pia kamanda wa kanda Maalumu jijini Dar es salaam ametoa taarifa ya Jeshi la polisi kumkamata

Freemasons anaefahamika kama Rajab Mohammed mwenye umri wa miaka 25 mkazi wa mwenge, Rajab amekuwa akiwakamata wanawake na kuwatishia kuwanyonya damu.

Lakini pia Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam limefanikiwa kumkamata Peter Kwema maarufu kama 'BABU' anaejihusisha na ujambazi katika mikoa ya DSM, Morogoro, Arusha,Tanga na Kilimanjaro

Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 maoni: