![]() |
| Advertisement |
Ikiwa zimepita takribani siku mbili tokea mrembo Nandy kuomba radhi kutokana na video yake ya faragha kusambaa mitandaoni, msanii Dogo Janja ameibuka na kudai wasanii hawana umoja na wanafiki huwa wanafurahi sana kuona mwenzao amepatwa na majanga ili mradi apotee katika tasnia.
Dogo Janja ametoa kauli hiyo usiku wa kuamkia leo Aprili 15, 2018 kupitia ukurasa wake maalumu wa kijamii na kusema anahisi anaweza kuchukiwa leo hii na wasanii wenzake ila ni lazima yeye aongee ukweli ili mradi donda ndugu liliopo katika muziki limepone.
Nahisi nnaweza kumaindiwa Leo na wasanii wenzangu ila lazima MTU aanze ndo hili donda ndugu litapona. Wasanii sisi ni masnichi sana aise, baada ya hii ishu ya nandy ndo nimepata uhakika. Wakati wa ishu ya Roma nilianza kuliona jinsi kwenye makundi pembeni watu kibao walikuwa wanafurahi tena maneno kibao kama atakoma, amezoea huyo...Jana na juzi nimekaa na watu wasanii wakubwa tu na wote walikuwa wanasema bora limemtokea nandy hili angalau spidi za show zitapungua...bora basata ingemfungia miezi 6 apotee kdg....walikuwa wanapiga story kama utani ila moyoni nimefikiria sana. Wasanii tuache roho mbaya, wote sisi maskini tunahangaikia ugali. Tukipata ajali kazini, tusiombeane mabaya tutafute amani...vita iwe kwenye kazi jamani. Hizi story za kufurahi ajali kazi mi nazikataa...
Video hiyo iliyosambaa wiki hii ilikuwa ikimuonesha Nandy akiwa Faragha na msanii billnas ambaye kwa sasa hayupo nchini
Kwa upande mwingine, Dogo Janja amewashauri wasanii wenzake wawe na moyo wa upendo kwa wenzao na waache tabia ya kufurahia matatizo wanayowapata wakiwa kazini.


0 maoni: