![]() |
| Advertisement |
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein amafanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mapinduzi kwa kuongeza Wizara moja zaidi, na kuwabadilishia Wizara baadhi ya Mawaziri.
Kufuatia mabadiliko hayo, shughuli za Vijana zimehamishiwa katika Wizara mpya ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo; shughli za Mazingira zimehamishiwa katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais; na shughli za Wakala wa Serikali wa Uchapaji zimehamishiwa Wizara mpya ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale.
Aidha, amewateua Naibu Mawaziri wapya wawili na kumbadilisha Wizara Naibu Waziri mmoja. Kufuatia mabadiliko hayo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hivi sasa itakuwa na Wizara 14 zenye Mawaziri na Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:
1. OFISI YA RAIS NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI
2. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi- Mheshimiwa Issa Haji Ussi Gavu
3. OFISI YA RAIS, KATIBA SHERIA, UTUMISHI WA UMMA NAUTAWALA BORA
4. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora – Mheshimiwa Haroun Ali Suleiman
5. Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora – Mheshimiwa Khamis Juma Mwalim
6. OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ZA SMZ
7. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ – Mheshimiwa Haji Omar Kheri
8. Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ – Mheshimiwa Shamata Shaame Khamis
9. OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS
10. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais – Mheshimiwa Mohamed Aboud Mohamed
11. Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais – Mheshimiwa Mihayo Juma Nhunga
12. WIZARA YA AFYA
13. Waziri wa Afya- Mheshimiwa Hamad Rashid Mohamed
14. Naibu Waziri wa Afya – Mheshimiwa Harusi Said Suleiman
15. WIZARA YA ARDHI, NYUMBA, MAJI NA NISHATI
16. Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati – Mheshimiwa Salama Aboud Talib
17. Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati – Mheshimiwa Juma Makungu Juma
18. WIZARA YA BIASHARA NA VIWANDA
19. Waziri wa Biashara na Viwanda – Mheshimiwa Balozi Amina Salim Ali
20. Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda – Mheshimiwa Hassan Khamis Hafidh
21. WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI
22. Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali – Mheshimiwa Riziki Pembe Juma
23. Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amal Mheshimiwa Mmanga Mjengo Mjawiri
24. WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
25. Waziri wa Fedha na Mipango – Mheshimiwa Dkt. Khalid Salum Mohamed
26. WIZARA YA HABARI, UTALII NA MAMBO YA KALE
27. Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale – Mheshimiwa Mahmoud Thabit Kombo
28. Naibu Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale – Mheshimiwa Choum Kombo Khamis
29. WIZARA YA KAZI, UWEZESHAJI, WAZEE, WANAWAKE NA WATOTO
30. Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto – Mheshimiwa Maudline Cyrus Castico
31. Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto –
Mheshimiwa Shadia Mohamed Suleiman
32. WIZARA YA KILIMO, MALIASILI, MIFUGO NA UVUVI
33. Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi – Mheshimiwa Rashid Ali Juma
34. Naibu Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi – Mheshimiwa Dkt. Makame Ali Ussi
35. WIZARA YA UJENZI, MAWASILIANO NA USAFIRISHAJI
36. Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji – Mheshimiwa Dkt. Sira Ubwa Mamboya
37. Naibu Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji – Mheshimiwa Mohamed Ahmada Salum
38. WIZARA YA VIJANA, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO
39. Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo – Mheshimiwa Balozi Ali Abeid Karume
40. Naibu Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo – Mheshimiwa Lulu Msham Abdulla
Aidha, Mheshimiwa Said Soud Said na Mheshimiwa Juma Ali Khatib
wanaendelea kuwa Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi na Mawaziri Wasiokuwa na Wizara Maalum.


0 maoni: