Jumatatu, 16 Aprili 2018

Mourinho "wachezaji waliobologa kutocheza dhidi ya Spurs

ad300
Advertisement

Wachezaji wa Manchester United ambao walishindwa  kufanya vizuri katika mchezo wa  Ligi Kuu ya dhidi West Brom hawatacheza mchezo wa FA   dhidi ya Tottenham, amesema kocha wa timu hiyo Jose Mourinho.

Mashetani wekundu walishindwa kufanya vizuri katika mchezo huo ambapo Manchester united ilifungwa  1-0 na West Brom huko Old Trafford siku ya Jumapili, na kupelekea Manchester City kutwaa  ubingwa wa ligi kuu nchini Uingereza

United atashuka tena dimbani siku ya jumatano kukipiga dhidi ya Bournemouth  kabla ya kukabiliana na Spurs.


Meneja  huyo kutoka nchini Ureno alisema "baadhi ya wachezaji ambao walicheza dhidi ya West Brom "hawana nafasi" katika mchezo dhidi ya Tottenham utakaopigwa katika uwanja wa Wembley.

Aliongeza kuwa  mchezo dhidi ya Bournemouth kwenye Uwanja wa Vitality itakuwa "nafasi kwa wachezaji wengine watakao cheza vizuri  kupata nafasi katika mchezo dhidi ya spurs

Alipoulizwa kufafanua kama alimaanisha wale waliofanya vibaya dhidi ya Baggies sasa hawatawakabili Spurs, Mourinho alisema: "Ndio.

"Ni vigezo gani kwa meneja anatumia kuchagua timu?

"Ninajua tu kiwango cha mmoja mmoja : ndiyo njia ninayotumia"

Mchezaji Ander Herrera aliondolewa katika mchezo dhidi ya West Brom, wakati Paulo Pogba alibadilishwa katika dakika ya 58.

Kuhusu Pogba, Mourinho alisema: "Hakuwa yeye tu na alikuwa na kadi ya njano, kwa hiyo alikuwa katika hali ngumu zaidi kuliko wengine.

"Na kucheza na wachezaji wawili tu wa midfield, huwezi kucheza na mchezaji mmoja katika hatari ya kutoweza kufanya makosa

"Unaweza kufanya hivyo ikiwa timu yako haijafungwa , lakini timu yetu ilikuwa imeshapoteza na mchezo wetu ulikuwa mgumu, kwa hiyo tulipoteza mipira mingi.

"Paulo  pogba alitolewa nje kwa sababu ya kadi ya njano, aliyopewa katika mchezo huo Siku ya jumapili

Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 maoni: