Ijumaa, 2 Machi 2018

Nikki wa pili azungumza baada ya nyimbo kufungiwa

ad300
Advertisement

Baada ya nyimbo kadhaa za wasanii wa muziki wa kizazi kipya kufungiwa Msanii na mkali wa rap kutoka kundi la weusi Nikki wa pili ameeleza na kusema kuwa nyimbo za matusi  ziliimbwa kwenye kampeni za uchaguzi akiandika kupitia ukurasa wa tweeter Nikki amesema

"Tukizungumzia nyimbo za matusi bana zilitoka wakati wa kampeni,  bwana we matusi ya nguoni, tena yakitukana watu wazima na heshima zao, hapa walezi walikaa kimya.

Lakini pia Nikki wa pili amewataka BASATA kutojikita kufungia  nyimbo za wasanii tu kwa sababu za kimaadili  Bali isimamie zaidi maslahi yao

Basata kama walezi,  msisahau pia kuyalinda maadili yetu ya kiuchumii,  kama mlezi alafu watoto wako wanakua wanaishia kufa, inamanisha hawa kulelewa vizuri kiuchumi

Hii karibuni nyimbo kadhaa za wasanii wa kizazi kipya zilifungiwa kutokana na kukosekana kwa maadili katika nyimbo hizo huku Msanii ROMA Mkatoliki akifungiwa kufanya muziki  kwa muda wa miezi sita

Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 maoni: