Jumapili, 25 Februari 2018

Mtibwa yaibuka kifua mbele kombe la shirikisho

ad300
Advertisement

Klabu ya soka ya Mtibwa sugar  yenye maskani yake Manungu Tuliani Morogoro leo imeibuka kidedea Mara baada ya kuichapa  bao 3 bila majibu klabu ya soka ya Buseresere yenye makao yake Mkoani Mwanza katika michuano ya Azam sports Federation cup
Mchezo huo uliopigwa katika uwanja wa nyamagana ilemela jijini Mwanza mbaka dakika 45 za kwanza kumalizika hakuna klabu iliyokuwa imeona lango La mwenzie
Kipindi cha pili klabu ya Mtibwa sugar ilianza kuonyesha mashambulizi yake na kupata goli la kwanza dakika ya 53 likipachikwa kimyani na mchezaji  hassani dilunga.
Kasi ya mchezo iliendelea Mtibwa sugar wakafanikiwa kuongeza bao la pili  kupitia kwa mchezaji wao Chanongo dakika ya  83 huku mchezaji Makalani akihitimisha idadi ya magoli katika mchezo huo kwa kuiongezea Mtibwa sugar bao la 3 na mchezo huo kuisha kwa Mtibwa sugar kuibuka kidedea kwa ushindi wa goli tatu kwa bila

Mtibwa sugar inakuwa timu nyingine inaopanda hatua inayofuata katika michuano hii Mara baada ya Njombe mji kupanda mwanzoni Mwa wiki hii

Mchezo mwingine naosubiriwa kwa hamu ni kati ya yanga na Majimaji utakaochezwa katika uwanja wa majimaji  mjini Songea Mchezo huu utahitaji timu moja itakayoungana na Mtibwa sugar na njombe mji katika hatua inayofuataa

Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 maoni: