Alhamisi, 10 Mei 2018

Sugu na Masongwa waachiwa huru

ad300
Advertisement
Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe.Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Mhe.Emmanuel Masonga wameachiwa huru leo jijini Mbeya.



Akizungumza baada ya kuachiwa huru Sugu amewashukuru wakazi wa Mbeya na wanachama wa Chadema kwa utulivu wao kipindi hicho alipikuwa akitumikia kifungo hicho

Joseph mbilinyi Sungu na Emmanuel Masonga walihukumiwa kifungo cha miezi mitano kwa kosa la  uchochezi dhidi ya serikali ya Raisi Dkt John pombe Magufuli alipokuwa katika mkutano wa hadhara mwishoni mwa mwaka jana

Walifungwa katika Gereza la Ruanda Jijini MbeyaHukumu hiyo ilitolewa Februari 26 mwaka huu



Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe ameongoza mapokezi yao. Akiongozana na viongozi na wanasiasa wengine wa chadema


Jeshi la Magereza limeeleza kuwa, Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi 'Sugu' na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Emmanuel Masonga wameachiwa huru kwa msamaha wa Rais, uliotolewa Aprili 26 mwaka huu, katika maadhimisho ya miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.


Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 maoni: