Jumatatu, 14 Mei 2018

Lulu kurudi Uraiani

ad300
Advertisement

Muigizaji wa filamu nchini Elizabeth Michael, maarufu Lulu, amebadilishiwa adhabu na sasa anatumikia 'kifungo cha nje' kwa amri ya Mahakama Kuu Tanzania.

Lulu alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela Novemba mwaka jana baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia msanii mwenzake, Steven Kanumba. 

Akizungumza na MCL Digital Jumatatu Mei 14,2018, Ofisa Habari wa Jeshi la Magereza, Lucas Mboje amesema Lulu amebadilishiwa adhabu na atatumikia kifungo cha nje kwa amri ya Mahakama Kuu ya Tananzia, Dar es salaam. 

"Lulu amebadilishiwa adhabu na ameachiwa juzi Jumamosi kati ya saa 2 hadi 3 asubuhi. Hii si kwamba ameachiwa huru, bali amebadilishiwa adhabu na atatumikia kifungo cha nje, kitaalamu tunaita ' Community service'' amesema Mboje 

Chanzo: Mwananchi 
Share This
Previous Post
Next Post

Pellentesque vitae lectus in mauris sollicitudin ornare sit amet eget ligula. Donec pharetra, arcu eu consectetur semper, est nulla sodales risus, vel efficitur orci justo quis tellus. Phasellus sit amet est pharetra

0 maoni: